Wednesday, December 31, 2014

To The Future.

Called to the future, 
The steps I make from here leave a mark
I want to be remembered, 
my story to be told for generations

Called to the future, 
I saw the signs
heard the summon
Chosen for a bigger world
Leaving home, growing wings
for soaring high and higher
tilI I feel the burn, like fire,
Motivation

My education begins here now
so I can do great things
but alone I know I cannot succeed
My brothers' hand I shall need, 
to help me wave that wand,
break free the chains,
bring light in the dark days,
My sisters' hand i need,
to help me change and shape my wrong ways, 
Wave that wand,
Save me from the spells of love,
those that seek to devour my soul, 
Come undress this foul;
Lies, deceit, arrogance,
Wave tha wand,
Break the violence.

Called to the future,
I need strength,
to hold his mighty's grace
Chosen for a bigger world
Given a chance -
a second chance to do better,
to soar higher against any weather,
to clean the mess of my past mistakes,
to right the wrongs my kind has made,
to find the forgotten and give them a voice,
to grant women the freedom of choice,
to bring back the dignity, 
stolen by those who've lost their humanity, 
to fight the evil of man's words,
shaking women, blinding them to forsaken their worlds
Yes I have been given a second chance to do it better,
and I shall soar higher against all weather.

Called to the future, 
Chosen for a bigger world,
When I get there do not ask me if I got money
ask me if I am proud
When I get there do not ask how many gigs
ask how many wins
because life is all about growth
So I shall wave that wand,
that pen I hold,
to clean the mess of my past mistakes,
to right the wrongs that my kind has made,
but alone I cannot succeed
for my brothers' hand
my sisters' hand
I shall always, always need.

(It's not the end of the year, but the beginning of a lifetime)
Bye 2014 welcome 2015.
©Zuhura Seng'enge
   29/12/2014.
(Please share, leave a comment)

Who Is To Blame?

Guilt, 
Guilt on their faces,
Shame in their eyes
Watching me cuffed to the pole, facing the judge
Freedom is not an option I'm a branded prisoner
Marked for my taste and style
Cursed by my own kind
The same ones who once told me I have never looked so fine
Then turned away and left me to die. 

Pain,
Pain in my chest,
Bloody tears in my eyes
Chained by the pole for every passerby to see
Left bare, left open, 
used as an object to raise fear
They call it education 101
I refuse to agree, 
How do we stand tall and say we are one? 
when we do not care for each other's lives
Friends, the community, intellectuals, the government;
You curse me, 
You curse my way of life
but you never cared to ask how I got that life
You shoot at me, bullet like words,
Venom that is tainting my name,
while it wasn't long ago you sat back and enjoyed the game
You battle me,
You push me down,
trowing me crosses
but you never tried to teach me how to bare a cross

So is it realy my fault?
If my parents did not raise me to be a lady
Is it realy my fault?
that globalization is taking over and our lives are turning over
Is It realy my fault?
That everyday cultures intergrate,
and our lifestyle they affect
Is it realy my fault?
That I'm a young girl with desires and
my peers' styles I admire
Is it realy my fault?
that this disease has lasted this long
Was I the first to wear a thong?
What was done to save youngsters when the first storm had blown?
Oow that's right,
You just laughed and minded your own
So is it realy my fault?
that our government was not strong enough to take action
that it was not strong enough to set direction
Is it my fault that the world is lost?

Silence was our best cup of tea
Ignoring all that was happening
but now that we're awake it's me that you see?
Blaming and condemning has become our best hobby
but there is so little we do to change our society
Yet we call ourselves intellectuals
We think ourselves righteous
We hold ourselves as patriots
except blaming and condemning,  what have we realy done
to create a better society from this rotten one?

©Zuhura Seng'enge
    12/12/2014.
(Please share, leave a comment)

Monday, December 29, 2014

SITAKI KUA MTUMWA.

" I'm your loyal servant! ''
Ulisema kwa ushupavu ukijiamini
Ukatia vionjo na ahadi nyingi
Kutupumbaza tusilione shombo
Kwenye kiti cha enzi ukila yamini
Kua utapiga vita rushwa na kutokomeza umasikini.
" I'm here to serve your needs! "
La hasha! Hukusimamia yako kauli
Ukaleta dharau na kiburi
Ukijitapa kwa nguvu na madaraka
Uliovikwa na unaowasulubisha
Nikatazama..
''A woman has no right to speak out! ''
Ikapigwa kampeni kwa tarumbeta
Wanawake tukakubali kukeketwa
Watoto wetu wakaachishwa shule mapema
Eti ni hasara kusomeshwa bora ya kuolewa
Tukakataliwa kujieleza na kuhitaji maendeleo
Tukafanywa kivutio cha biashara na vileo.
''A woman was born to serve a man! ''
Nyimbo tukaimbishwa tukumbuke hata usingizini
Tukafanya mazoea maisha yetu kutothamini
Tukakubali kunyanyaswa matope tukayaramba
Wakila zao kuku bata sisi tunakesha shamba,
Nikanyamaza..
''You are the only one for me! ''
Ukanipamba nikakubali kudanganyika
Kwa mapenzi ya kinafiki kila siku ukanizuga
Nikazama kwenye shimo la kenge na mamba
Majeraha nikayavaa nikazidi kuvuta kamba
Kwani kwako nilipenda
Na kwako nikachuma vidonda.
''You are more beautiful in a mini skirt! ''
Ati fasheni ndio alama ya uzuri wangu kwako
Nisipokaa uchi sio wa matawi kwako
Nisipojua kula bata siwezisimama pembeni yako
Nisipoweza kukatika siwezipata penzi lako
Nikakubali kunuka shombo
Nikidhani uzuri ni ule wa macho
Nikakufanya wangu mwandani
Kumbe kwako nimekua makombo
Nikakubali..
Nimeishi kwenye giza la utumwa wa nchi,
Utumwa wa nafsi, utumwa wa mwili
Ninajua mimi sio kiumbe kamili
Ila sitokubali kuendelea kuzama majini
Nimetazama ahadi zikivunjwa
Na wale niliowaamini kunitunza
Wakaapa kuongoza kwa haki
Kisha wakala mali zetu tukabaki kuuza mishikaki
Nimenyamaza wakati ninadhulumiwa
Elimu yangu kuonekana udhia
Maisha yangu kuwekwa kwenye mizani
Na wengine ndio wa kuyatia ama kutoa thamani
Nikakubali kuweka imani juu ya yule mtu
Anaependa kukosoa, asiethamini utu
Ambaye mapenzi kwaye ni mashindano
Anayefanya uzuri biashara ya mitandao.
Nimetazama!
Nikanyamaza!
Nikakubali!
Kuonewa na niliowaamini kwa moyo
Wakieneza gonjwa la woga katika jina la upendo
Sitaki tena kua mtumwa wa wanafiki na waongo
Sikubali kunyamaza kimya na kuwageuzia mgongo
Mkuki watanichoma nikiwa sina habari
Ila sasa nimewasoma sizami tena bahari.
©Zuhura Seng'enge.
  29/12/2014.
'' Slavery takes many forms. Beware of people who love you for your fame and your face, for they will always belittle your strengths.
He who loves you seeks not to possess you but to bring out the best in you.''
(Please share, leave a comment)

Thursday, December 25, 2014

KAMA KIJANA HURU.

Kama kijana huru ninashukuru
Mungu kwa kuzaliwa kipindi uhuru umeshaingia
Kwa kulikuta taifa limeshazaliwa
Kwa kuikuta amani imeshajengeka
Kama kijana huru ninashukuru
Mashujaa walioipigania na kutetea uhuru
Viongozi, wanajeshi na wananchi waliojitoa kila siku
Wakayaona mauti na bado wakazidi kuchonga mikuki
Wakapigwa mijeledi na bado wakashika bunduki
Kama kijana huru ninashukuru
Waliotangulia kabla yetu kwa jasho na damu
Walilomwaga kukataa ukoloni wakavikwa utumwa
Wakashuhudia watoto wao wakivuliwa utu na kupigwa mitama
Kama kijana huru ninashukuru
Mungu kuzaliwa kipindi cha uhuru.

Kama kijana huru ninajukumu
La kuthamini utu na maisha ya mtanzania mwenzangu
La kuendeleza hekima na busara za waliopita kabla yangu
Waliojua maana ya uzalendo na
Wakajenga nchi kwa vitendo
Kama kijana huru ninajukumu
La kutetea haki za msingi za mtanzania mwenzangu
La kuhakikisha demokrasia ya maneno inaangamizwa kwa nguvu
Na vijana wa kitanzania wanaacha uvivu
Kama kijana huru ninajukumu
La kupambana na maadui wa maendeleo ya mtanzania
Ikiwemo ufisadi, rushwa, ubaguzi na imani za kishirikina
La kuelimisha jamii na kuifungua macho
Kua maana ya kua huru ni kuthamini na kuendeleza kidogo ulichonacho
Kua ujinga na kupuuzia uovu ndio chanzo cha machafuko
Kama kijana huru ninajukumu
La kuendeleza amani, upendo na uhuru.

Kama kijana huru ninahaki
Ya kujua ukweli na sio kuwekwa gizani
Ya kupata vizuri bila kupimwa mizani
Ya kupinga uonevu hasa kwa wanyonge na masikini
Ya kudai uhuru wangu, na mchango wangu kuuthamini
Kama kijana huru ninahaki
Ya kutimiziwa haki zangu za msingi;
Elimu bora, afya bora, usalama wa maisha na mali
Ila yasikitisha kuona zinazidi kudorora hali
Huduma mbovu, mishahara midogo na elimu ya dafutari
Kama kijana huru ninahaki
Ya kujua miaka 53 ya uhuruImenipa nini
Na kutambua kwa miaka 53Ninajivunia kitu gani.

©Zuhura Seng'enge 
  09/12/2014.

(Please share, leave a comment)

Monday, December 8, 2014

UNAFURAHIA KUA MTANZANIA HURU?

Tanganyika huru,

Ndilo lilikua lengo kuu la baba wa taifa

Tanganyika shujaa,

Ndio uliokua msimamo mkuu wa baba wa taifa

Tanganyika endelevu,

Ndio iliokua jitihada kuu ya baba wa taifa

Na ujinga, maradhi, umasikini

Ndio yaliyokuamapambano makuu ya baba wa taifa.

Ni miaka 53 tangu uhuru utangazwe Tanganyika
Mwalimu alijitoa kuhakikisha tunasonga mbele watanganyika
Katika kipindi cha uhai wake alisisitiza sana juu ya upendo na umoja
Akijua Ipo siku yeye na sisi hatutokua tena pamoja
Tukaapa kuyafuata mafundisho aliyotuasa
Tukaahidi kutekeleza maagizo aliyoyaacha
Kwa machozi tena ya kwikwi, tukimkufuru hadi na Mungu

Tukatoa vyetu viapo, 'Tanganyika shujaa, Tanganyika huru'

Na tukasema kwa kishindo, 'Mtanganyika kabla ya mzungu'

Wanafiki!!

Tulijipamba kwa tabia nzuri mbele ya macho ya watu
Tukafuata kama kondoo wema kumbe asili yetu ni chatu
Ahadi nyingi tukazitoa na mipango lukuki lukuki
Watanzania bila kujua wakaukumbatia mkuki
Tukawa sababu ya taabu na dhiki
Tukajenga kati yetu chuki
Ujinga, maradhi, umasikini, vikatawala jamii zetu
Na sasa vimezaa watoto, wanaotawala maisha yetu;
Siasa chafu, ufisadi, rushwa, ujambazi, uvivu, unyanyasaji
Udini na ukabila, imani za kishirikina, ukatili na mauaji
Ndizo zimekua wimbo wa taifa
Nasi tumekaa tukitazama watoto wetu wakiangamia
Maradhi haya yakijenga donda ndugu katika nafisi zetu
Katika maisha yetu.

Tanzania huru, Tanzania shujaa, Tanzania endelevu
Lengo la mwalimu
Leo miaka 53 maadhimisho ya siku yetu
Tunajivunia kitu gani katika kua huru?
Zaidi ya kuongeza na kudai ushuru
Zaidi ya kutia giza kwenye nuru
Maendeleo? Ndio yapo kadhaa
Je yana thamani gani kama bado tunakufa na njaa?
Je yana thamani gani kama utu, upendo, umoja na ukweli ndio yetu karaha?

Tafakari, chukua hatua.
Hongera kwa kuiona miaka 53 ya uhuru Tanzania bara.

©Zuhura Seng'enge.
  09/12/2014.

(Please share, leave a comment)

NITAMPIGANIA MWANAMKE.

Nimejawa huzuni, majonzi mengi moyoni
Dukuduku langu la siri ni kama kitanzi shingoni
Kifua changu kilichokua hifadhi ya mambo mengi, leo chakataa kutunza siri
Hakika huu ni udhalili
Macho yangu yaliojawa upendo na upole, leo yanachoma kama mishale
Machozi tele kwa tele
Sikujua ukimya wangu unaweza kua silaha
Ya kuongeza uovu na kupora amani na furaha
Sasa nimechoka kutazama wenzangu wakiumia
Nimechoka kuyafuta machozi yao wakilia
Nimechoka kuhudhuria misiba yao wakiangamia
Leo nasimama kupigania
Uhuru na utu wa mwanamke
Leo nasimama kutetea
Haki za msingi za mwanamke
Najitoa kumpigania mwanamke.

Nilijawa wasiwasi na hofu nyingi moyoni
Dukuduku langu la siri likanitia majutoni
Nilidhani nitavumilia na maisha yatasonga mbele
Ila kwa hakika nilipotea kwani mateso ndio yakazidi kujenga kilele
Sasa sitosubiri miujiza kutoka kwa Mungu
Nitashika risasi, jambia hata na rungu
Kupambana na adui alieleta hofu na kiza
Akamfanya mwanamke kibwagizo na kivutio cha kuingiza fedha
Leo nasimama  kupingana na dhana za mfumo dume
Nasimama kupigana na anaejiita baba, kaka, ndugu, jamaa na mume
Kisha akaweka majeraha ya wazi na siri kwenye maisha ya mwanamke
Nasimama kukemea ukatili kwa nguvu zangu zote
Nimechoka kuweka siri, kwani siri ya ugonjwa ni mauti
Sasa najitoa kumpigania mwanamke kwa yangu sauti.

I say No to violence today!

©Zuhura Seng'enge.
     08/12/2014.

(Please share, leave a comment)

#16 days of Activism~ SAY NO TO VIOLENCE.


For many years women and girls all over the world have been subjected to brutal acts of violence;
Sexual harassment, battery, their lives used as amusement to the world of men.
For many years women and girls have endured this embarrassment from their family members, syblings, strangers.Their lips were sealed forbidden to speak out. Sometimes their children used as leverage for their silence, and for so many years they have kept this secret and many died with it.

For so many years fear has been our best friend keeping us from seeing the true strength and power that we wield. We have been called names; prostitutes, harlots, filthy creatures, good for nothing, men's entertainment. We have endured it all and for a twisted reason we accepted to be objectified and subjected to this humiliation because we thought we deserved it. We thought it was fitting, that we were born weak beings to be driven by men's desires. How wrong we were, and how wrong we are if we still believe this.

For some time now the song has been the same, we 'want freedom of choice', 'we want love', 'we want respect' but have we tried to demand it? It is ours to have, our birthright not something we should earn.
So today I say stop singing, hold a banner and scream it. Today I say stop dreaming, wake up and live it. Today, women and girls from all over the world shall no longer endulge men and their twisted minds, women and girls shall no longer endulge fear and silence. We shall rise together, scream together, fight together, fight for eachother, to demand our birthright, our freedom from coercion. To demand our birthright, our right to a peaceful life, a happy life, a healthy life.

For many years women and girls all over the world have been subjected to brutal acts of violence..
but that time is now over. It is time to break the silence, and say NO to violence.
So say NO! To violence.

Zuhura Seng'enge.

(Please share, leave a comment)

Thursday, December 4, 2014

KEMEA UKEKETAJI.

Mwanamke wa Tanzania ana haki,

Mwanamke wa Tanzania ana nafasi,

Mwanamke wa Tanzania ana sauti.

Awe mjumbe wa vitongoji vyote,

Awe mtetezi wa wanawake wote,

Awe imara, tayari siku zote,

Kukemea dhana potofu za unyanyasaji,

Na vitendo hatari vya ukeketaji.

Linda afya yako, linda hadhi yako,

Jipende,

Kataa kukeketwa!!

Zuhura Seng'enge.
25/11/2014.

(Please share, leave a comment)

YA DUNIA.

Nimechoka kuvumilia, maudhi haya,
Nimechoka kusikia, wanawake wakilia,
Kila kona ya dunia, watoto wanaumia,
Nimechoka kupokea, 
Lawama na vitisho,
Kila ninapoangalia, ni mauaji ya albino,
Watu wanateketea;
Ubakaji, ukeketaji, unyanyasaji wa jinsia,
Utu umeshapotea.

Rushwa nayo yachochea, watu kesi kuzushiwa,
Vijana, wazee, madawa kuyatumia,
Afya zao kujihatarishia,
Bidhaa za bei chee, ndizo tunang'ang'ania,
Nyingi feki twasikia, bado tunakazania? 
Iko wapi ile nia, ya maisha kujijengea? 
Tumezongwa na dunia;
Wadada kusaka pesa, wakaka kuuza sura
Viwanja kujitanua, elimu kuipu'za.

Nao wenye nyingi ndoto, kazi hawashikilii
Hawaachi kupiga zogo, wakazisaka rupia,
Wanazidi likosa soko, maisha kuyajutia
Mengi nayafikiria, yaumiza watanzania,
Nimechoka kuvumilia, maudhi nazo ghasia,
Haki naitamania, amani ninaililia,
Wazazi nipeni elimu, niyashinde ya dunia
Wazazi nipeni elimu, isinishinde dunia.

Zuhura Seng'enge.
02/10/2014.
(Please share, leave a comment)

KWAKO NINATAMANIA.

Asubuhi inapofika maswali mengi hunijia
Wapi nitakwenda?
Nini nitakula?

Nikitangatanga kiguu na njia
Jua nalo likianza kusogea
Najiuliza wapi nitaanzia
Mawazo yanivaa na kutonesha vidonda

Maisha ya zamani nayatamania
Niliishi kwa amani sikuwahi fikiria
Kama shilingi mia itakua adimu,
Kama mkate ulooza nitalilia.

Usiku unapoingia hofu nyingi hunikaribia
Nani atanidhuru?
Wapi nitajilaza?

Ninaangaza huku na huko
Kutafuta hata boksi na mfuko
Tumbo likiunguruma kwa njaa
Ni siku ya tatu sasa, naanza kukata tamaa

Mvua ikininyeshea nimekaa pweke nikilia
Miaka sita nipo kitaa ndoto zangu zinanikimbia.

Asubuhi inafikia na huzuni yanivamia
Safari nyingine kiguu na njia
Kutafuta pakufikia

Nikigonga kwako nipokee
Hata shilingia mia nitolee
Nipate maji na andazi
Nisijechetuka nikafa jambazi.

Ewe unayetupa chakula
Huogopi hata Mungu?
Wengi tunakililia
Tulikombe hata jungu.

Usione udhia.

Zuhura Seng'enge.
20/11/2014.

(Please share, leave a comment)

MAISHA BILA HEKIMA.

Maisha bila ya heshima,
Hujawa maovu daima,
Maisha bila ya hekima,
Ni yenye upotovu lazima,
Enyi kaka na dada zangu, 
Hifadhi yangu ni yenu pia,
Heshima mnaponivulia,
Na zenu doa hutia,
Mama zetu, baba zetu,
Fungueni macho, sikia,
Tusipoacha puuzia,
Maovu hayataishia,
Tupambane na mtazamo,
Sio na masakamo,
Mnielimishe, msiniaibishe
Tofauti zetu tusawazishe,
Kwani maisha bila ya hekima,
Ni yenye upotovu daima.
©Zuhura Seng'enge
   23/11/2014.
(Please share, leave a comment)

NAJIVUNIA KUWA MTANZANIA

Tanzania! Tanzania!
Nchi yangu naipenda
Kuwa mtanzania ninafurahia
Kiswahili lugha yetu ndio
Yatuunganisha
Amani fahari yetu ndio
Yatupatanisha
Ninajivunia mimi kuwa mtanzania
Na kiswahili changu ndio ninaringia.

Mimi ni mtanzania
Nchi yangu naishangilia!
Kila sifa imejaaliwa
Upendo, mshikamano, ndio nguzo yetu kuu
Natembea kifua mbele
Popote niandapo macho huku na huku
Kwasababu najivunia mimi kuwa mtanzania
Na kiwsahili changu ndio ninaringia.

Tangu enzi na enzi kiswahili umoja wetu
Mbali kimetutoa kikaleta uhuru wetu
Nasema ahsante Mungu
Kwa kuzaliwa mtanzania
Nyumbani kwetu pazuri wageni
Wanang'ang'ania
Nguo zetu za asili tukivaa tunavutia
Nyimbo zetu ni mwanana tukiimba
Ndege wanashangilia
Watoto wanafurahia
Ninajivunia mimi kuwa mtanzania
Na kiswahili changu ndio ninaringia.

Bendera yetu ya taifa, wimbo wa taifa
Mqenge wa uhuru, ndio nembo zetu
Afrika na duniani pote
Ndizo zatutambulisha
Tanzania, Tanzania
Nakupenda Tanzania
Zana zetu, mapambo yetu
Kazi ya mikono yetu
Sanaa zetu ni burudani
Na elimu kwa jamii yetu
Tujivunie asili yetu
Mzizi wa utamaduni wetu
Tujivunie sisi kuwa watanzania
Na kiswahili chetu kukiringia.

Zuhura Seng'enge.
04/12/2014.

(Please share, leave a comment)