Thursday, June 16, 2016

Watoto Ndiyo Taifa



Natamani kuwa na jamii yenye amani
Niione machoni
Isiishie ndotoni,
Jamii ambayo watoto wana furaha
Wakiimba na kucheza
Hadithi kusimuliana,
Mahali watakapopendwa na wazee na vijana
Mahali watakapokuwa salama,

Jitihada za maisha bora ziwe kwa watoto
Wapate urithi kwa kzazi kijacho.

Natamani kuwa na jamii watakayopendwa watoto
Isiyotumia maumivu yao
Kuzichuma mali,
Natamani kuona wakipata haki zao
Mahali tabasamu lao
Litathaminiwa kuliko dhahabu,
Wasipotumikishwa wala kufanywa kama bidhaa
Wasipotelekezwa wakaja kufa kwa njaa
Wakiwa pweke kwenye dunia,
Natamani jamii itakayo wajali
Ikawaweka mbali na vitendo vya ukatili.

Natamani kuwa na jamii watakayothaminiwa watoto
Mahali Sauti zao
Zitasikiwa na wote,
Elimu yao kupewa kipaumbele
Mahali wasipolazimishwa
Kuuvunja undugu,
Na akili zao kutopotoshwa kwa uongo
Chuki ikajaa mioyoni mwao
Wakasahau kuwa na upendo,
Natama jamii ambayo watoto wataishi bila woga
Mahali salama penye tumaini na faraja.

Watoto ni baraka kwenye maisha,
Watoto ndiyo nuru kwenye kiza,
Watoto ni tumaini, watoto ni zawadi
Watoto ndiyo taifa.

*Translated From English

(c) Zuhura Seng'enge
        ~ A. L 2016
www.Zuhurasaad22.blog spot.com



No comments:

Post a Comment

Please share your thoughts and feelings..