Thursday, December 4, 2014

YA DUNIA.

Nimechoka kuvumilia, maudhi haya,
Nimechoka kusikia, wanawake wakilia,
Kila kona ya dunia, watoto wanaumia,
Nimechoka kupokea, 
Lawama na vitisho,
Kila ninapoangalia, ni mauaji ya albino,
Watu wanateketea;
Ubakaji, ukeketaji, unyanyasaji wa jinsia,
Utu umeshapotea.

Rushwa nayo yachochea, watu kesi kuzushiwa,
Vijana, wazee, madawa kuyatumia,
Afya zao kujihatarishia,
Bidhaa za bei chee, ndizo tunang'ang'ania,
Nyingi feki twasikia, bado tunakazania? 
Iko wapi ile nia, ya maisha kujijengea? 
Tumezongwa na dunia;
Wadada kusaka pesa, wakaka kuuza sura
Viwanja kujitanua, elimu kuipu'za.

Nao wenye nyingi ndoto, kazi hawashikilii
Hawaachi kupiga zogo, wakazisaka rupia,
Wanazidi likosa soko, maisha kuyajutia
Mengi nayafikiria, yaumiza watanzania,
Nimechoka kuvumilia, maudhi nazo ghasia,
Haki naitamania, amani ninaililia,
Wazazi nipeni elimu, niyashinde ya dunia
Wazazi nipeni elimu, isinishinde dunia.

Zuhura Seng'enge.
02/10/2014.
(Please share, leave a comment)

No comments:

Post a Comment

Please share your thoughts and feelings..