Friday, January 2, 2015

Tufurahi.

TUFURAHI.
Umebadili maisha yangu,
Ukauteka na moyo wangu,
Mapenzi yako asali yangu,
Amani na furaha ni nyingi ukiwa kwangu.


Uzima wako faraja yangu,
Ucheshi wako liwazo langu,
Ukweli wako heshima yangu,
Nitunze nikutunze daima ukae kwangu.

Tusisikilize yale ya watu,
Kuaminiana jukumu letu,
Kusalitiana tusithubutu,
Tufurahi kila siku upendo ukae kwetu.


Tuwe kitu moja tupange yetu,
Tukishikamana ushindi wetu,
Tukivumilia mavuno yetu,
Tumuombe nae Mungu mazuri yapite kwetu.

©Zuhura Seng'enge
    01/10/2014.

(Please share, leave a comment)

No comments:

Post a Comment

Please share your thoughts and feelings..